Welcome to this forum, where you can xpress your views limitlessly. it's a platform where you can exercise your right as provided under Article 18 of the constitution of United Republic of Tanzania 1977. Academics and social aspects debatable are warmly welcomed. it's a non partisan however.
Thursday, March 6, 2014
CHRISTIANO RONALDO SASA NDIO MFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA URENO
Mwanasoka bora wa dunia na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo ameandika historia mpya katika soka jana usiku kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Cameroon ambapo Ureno walishinda mabao matano kwa moja.
Ronaldo ambaye alifunga mabao mawili kwenye mchezo huo yaliyomfanya kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno aliyefunga mabao mengi zaidi katika historia ya timu hiyo ya taifa.
Winga huyo wa Real Madrid sasa amefikisha jumla ya mabao 49, mawili zaidi ya Pauleta ambaye alikuwa anashikilia rekodi ya kufunga mabao huko nyuma.
Listi ya wafungaji bora wa muda wote wa Ureno
1. Cristiano Ronaldo (109 caps) - 49 goals
2. Pauleta (88 caps) - 47 goals
3. Eusebio (64 caps) - 41 goals
4. Luis Figo (127 caps) - 32 goals
5. Nuno Gomes (79 caps) - 29 goals
Subscribe to:
Posts (Atom)