Tuesday, June 14, 2011

Jike na Dume wafunga ndoa;

be the first to know..

Harusi ya mbwa huko majuu;

Harusi
Harusi ya mbwa

Kuna msemo usemao, kila mbwa ana siku yake. Na msemo huu umedhihirika, sio kwa mbwa mmoja bali wawili hapa Uingereza.
Mbwa hao ambao majina yao ni Pete na Zoe, wenye umri wa miaka mitano, wanatarajiwa kufunga ndoa hivi karibuni. Gazeti la The Sun limeripoti kuwa wawili hao wanaoishi katika nyumba ya kulelea wanyama wa mitaani, watafanya harusi yao katika ukumbi wa kituo cha wanyama cha Wood Green huko Godmanchester, Cambridgeshire.
Harusi hiyo ya aina yake itahudhuriwa na wafanyakazi wa kituo hicho, wananchi wa kawaida na marafiki wa karibu wa mbwa hao, ambao pia ni mbwa. Ndoa hiyo itafungishwa na Kasisi Gael Lees wa kitengo cha kulelea paka cha hapo Wood Green, ambaye atasoma ahadi maalum zilizoandikwa kwa ajili ya mbwa hao.
Baada ya harusi hiyo, mbwa harusi hao watarejeshwa katika makazi yao na kupatiwa keki yenye ngazi tatu iliyotengenezwa kwa maini ya ngombe, na bakuli la maji. Bwana harusi wa mbwa, bila shaka ataitwa.. Mbwana harusi, bibi harusi je..??

funny fella in the Bus;

be the first to know..



      kumbe, kunambinu nyingi za mwizi kuiba!
Polisi nchini Uhispania wamemkamata bwana mmoja mwenye mwili unaoweza kunyumbulika kwa makosa ya wizi.
Mwizi huyo inadaiwa alikuwa akijificha ndani ya sanduku, na sanduku hilo kuwekwa katika mizigo ya abiria kutoka uwanja wa ndege wa Girona wanaokwenda jijini Barcelona. Kwa mwezi mzima polisi walikuwa wakishangazwa na wizi unaotokea kwenye eneo la kuwekea mizigo ndani ya basi. Hivi karibuni wizi kama huo ulitokea tena ambapo masanduku yote ya abiria yalikuwa yamevunjwa na vitu kuibiwa.
Hata hivyo abiria mmoja aligundua kuwa sanduku moja tu ndio lilikuwa halijaguswa. Polisi waliitwa na walipofungua sanduku hili walimkuta mtu amejikunja ndani yake. Polisi pia walimkamata mwenzake na mwizi huyo ambaye alikuwa akimpeleka kama mzigo ndani ya basi hilo.
Mwenzi huyo alikuwa akinunua tiketi ya basi na kuweka sanduku lake hilo lenye mwizi mwenzake katika eneo la mizigo, ambapo wakiwa safarini, mwizi huyo hutoka ndani ya sanduku na kuanza kuvunja na kuiba masanduku ya abiria.
Kabla ya mwisho wa safari, bwana huyo mwenye mwili unaonyumbulika, alikuwa akiingia katika sanduku lake na kujifungia ndani tena, na kubaki kama mizigo mingine.

              ZE great;