Tuesday, June 14, 2011

Jike na Dume wafunga ndoa;

be the first to know..

Harusi ya mbwa huko majuu;

Harusi
Harusi ya mbwa

Kuna msemo usemao, kila mbwa ana siku yake. Na msemo huu umedhihirika, sio kwa mbwa mmoja bali wawili hapa Uingereza.
Mbwa hao ambao majina yao ni Pete na Zoe, wenye umri wa miaka mitano, wanatarajiwa kufunga ndoa hivi karibuni. Gazeti la The Sun limeripoti kuwa wawili hao wanaoishi katika nyumba ya kulelea wanyama wa mitaani, watafanya harusi yao katika ukumbi wa kituo cha wanyama cha Wood Green huko Godmanchester, Cambridgeshire.
Harusi hiyo ya aina yake itahudhuriwa na wafanyakazi wa kituo hicho, wananchi wa kawaida na marafiki wa karibu wa mbwa hao, ambao pia ni mbwa. Ndoa hiyo itafungishwa na Kasisi Gael Lees wa kitengo cha kulelea paka cha hapo Wood Green, ambaye atasoma ahadi maalum zilizoandikwa kwa ajili ya mbwa hao.
Baada ya harusi hiyo, mbwa harusi hao watarejeshwa katika makazi yao na kupatiwa keki yenye ngazi tatu iliyotengenezwa kwa maini ya ngombe, na bakuli la maji. Bwana harusi wa mbwa, bila shaka ataitwa.. Mbwana harusi, bibi harusi je..??

No comments:

Post a Comment

please use the appropriate language to comment. Ze great respects comments from his esteemed readers. thanks for visting this blog.